Breaking News
Loading...
30 Nov 2013

Ethiopia na Kenya zashinda CECAFA

Timu ya taifa ya Ethiopia al maarufu "Walya Antelopes" na timu ya taifa ya Kenya "Harambee Stars" ambazo zipo kundi A zimeshinda mechi zao kwenye mashindano ya CECAFA Senior Challenge Cup siku ya jumamosi.

Ethiopia kwa upande wao waliiadhibu Zanzibar kwa jumla ya magoli ya 3 - 1 huku "Harambee Stars" ikibamiza bila huruma Sudan Kusini kwa jumla ya magoli 2 - 1.
Katika mechi ya ufunguzi siku ya jumatano wakati Kenya na Ethiopia zilipokutana zilitoka sare ya bila kufungana huku Zanzibar wao walifunga Sudan Kusini kwa jumla ya magoli 2 -1.
Kundi A linajumuisha Kenya, Ethiopia, Sudan kusini na Zanzibar wakati kundi B lina timu ya Tanzania, Zambia, Burundi na Somalia huku kundi C likihusisha mabingwa watetezi Uganda, Rwanda, Sudan na Eritrea.

Siku ya Jumapili kulitarajiwa kuwa na mechi ya kundi B ambapoTanzania na Somalia zilitarajiwa kumenyana vikali katika mechi ya awali majira saa 8:00 mchana kwa saa za Afrika Mashariki. Mechi nyingine ya kundi B Zambia ambao ni timu mwalikwa ilitarajiwa kupambana vikali na timu ya taifa ya Burundi.

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2013 Bring 255 | Exclusive Blogging Experience All Right Reserved